http://www.swahiliebgc4lpd7xcpitlp6ilzdgk6atnhnzqohywcgtr7jbcrq6fqd.onion/a/miili-mingine-29-yafukuliwa-katika-ya-msitu-wa-shakahola/7091695.html
Mackenzie bado hajatakiwa kujibu mashitaka, lakini mahakama iliamuru Jumatano azuiliwe kwa wiki tatu nyingine wakisubiri uchunguzi zaidi kuhusu kile kinachoitwa "Mauaji ya Msitu wa Shakahola". Mwanzilishi huo wa Kanisa la Good News International mwenye umri wa miaka 50 alijisalimisha tarehe 14 Aprili, baada ya polisi kwanza kudokezwa na kuingia katika msitu wa Shakahola.